Join Us on WhatsApp JIUNGE NASI WHATSAPP
Uhakika News
  • Home
  • MICHEZO
    • Mikeka ya leo
  • AJIRA KAZI
  • NYIMBO MPYA YA
  • ELIMU
    • JKT selection
    • Form One Selections
    • form five selections
    • NECTA Form Six Results
    • NECTA Standard Seven Results
No Result
View All Result
AI News
  • Home
  • MICHEZO
    • Mikeka ya leo
  • AJIRA KAZI
  • NYIMBO MPYA YA
  • ELIMU
    • JKT selection
    • Form One Selections
    • form five selections
    • NECTA Form Six Results
    • NECTA Standard Seven Results
No Result
View All Result
UK News
No Result
View All Result

Prof. Nombo Azindua Miongozo Utoaji Mikopo na Ruzuku kwa Mwaka 2025/2026

by Mr Uhakika
June 16, 2025
in HESLB
Reading Time: 3 mins read
A A
Share on FacebookShare on Twitter
Table of contents
  1. You might also like
  2. Awamu ya kwanza Majina ya Wanafunzia walipata mikopo na ruzuku yenye jumla ya wanafunzi 135,240
  3. Orodha ya Majina Ya Waliopata Mkopo HESLB Batch 1, 2 & 3 – Pakua PDF 2025/26
  4. Share this:
  5. Related
Join Us on WhatsApp KARIBU UJIUNGE NASI WHATSAPP

Dodoma, Ijumaa, Juni 6, 2025

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia (WyEST), Prof. Carolyne Nombo leo (Ijumaa, Juni 6, 2025) amezindua miongozo ya utoaji mikopo na ruzuku kwa wanafunzi wa elimu ya juu na vyuo vya kati kwa mwaka 2025/2026 kuanzia ngazi ya Stashahada hadi Shahada za Juu.

You might also like

Awamu ya kwanza Majina ya Wanafunzia walipata mikopo na ruzuku yenye jumla ya wanafunzi 135,240

Orodha ya Majina Ya Waliopata Mkopo HESLB Batch 1, 2 & 3 – Pakua PDF 2025/26

Katika hotuba yake iliyoandamana na uzinduzi rasmi wa miongozo hiyo, Profesa Nombo amesema miongozo hiyo itachapishwa katika tovuti za HESLB na WyEST ili kuwapa fursa waombaji mikopo na wadau wengine kusoma miongozo hiyo kabla ya dirisha la uombaji mikopo kufunguliwa.

“Miongozo itaanza kupatikana kwenye tovuti ya Wizara ya Elimu (www.moe.go.tz) na tovuti ya Bodi ya Mikopo (www.heslb.go.tz). Ninawashauri wanafunzi, wazazi na walezi waisome na kuzingatia maelekezo yaliyomo”, amesema Prof. Carolyne Nombo.

Hafla ya uzinduzi imefanyika katika ukumbi wa Seneti wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) ambapo wadau mbalimbali akiwemo Makamu Mkuu wa Chuo cha UDOM Prof. Lughano Kusiluka ameshiriki na kusema chuo hicho ni miongoni mwa vyuo ambavyo wanafunzi wake wananufaika na mikopo na ruzuku zinazotolewa na serikali kupitia HESLB.

Wadau wengine walioshiriki katika hafla hiyo walikuwa viongozi wa Shirikisho la Wanafunzi wa Vyuo vya Elimu ya Juu na Kati (TAHLISO na ZAHILFE), Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA), Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA), na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF).

Awali, akitoa neno la utangulizi, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB, Bw. Elihuruma Lema amesema kuwa HESLB imejiandaa na iko tayari kupokea maombi ya mikopo ya wanafunzi kuanzia Juni 15, 2025 hadi Agosti 31, 2025.

“Kuanzia Juni 15, 2025, mwombaji atapaswa kuingia kwenye tovuti ya HESLB www.heslb.go.tz kisha atabofya kiunganishi ‘Loan Application’ kwa kutumia Namba ya Kidato cha Nne na kufuata maelekezo. Mwisho wa kupokea maombi ya mikopo utakuwa Agosti 31, 2025 amesisitiza Mkurugenzi Lema.

Miongozo ya utoaji mikopo na ruzuku kwa wanafunzi iliyozinduliwa leo ni maandalizi ya kupokea maombi na hatimaye kupanga mikopo kwa wanafunzi wahitaji wenye sifa. Miongozo hiyo ni ya Stashahada (Diploma), Shahada za awali (Bachelor Degree), Stashahada ya Juu ya Sheria kwa Vitendo (Law School), Shahada za Uzamili na Uzamivu, na  Ruzuku (Samia Scholarship).

Katika kipindi cha miaka minne iliyopita (2020-2021 hadi 2024-2025), Serikali imeongeza bajeti ya fedha za mikopo ya elimu kutoka TZS 464 bilioni (2020-2021) hadi TZS 787 bilioni mwaka unaomalizika wa 2024/2025. Katika mwaka mpya wa masomo 2025/2026 utakaoanza mwezi Oktoba, 2025, bajeti iliyoidhinishwa ni TZS 916.7 bilioni inayotarajiwa wanafunzi 252,773.

Share this:

  • Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
  • Click to share on X (Opens in new window) X

Related

Tags: HESLB
ShareTweetPin
JE UNA MASWALI? JIUNGE NASI WHATSAPP
Previous Post

Jinsi ya kupata mkopo wa Elimu ya Chuo Tanzania

Next Post

IFM online application; Jinsi ya kufanya maombi ya chuo cha IFM 2025/2026

Mr Uhakika

Mr Uhakika

Related Stories

Maombi ya mkopo HESLB OLAMS – Online Loan Application 2025/26 – HESLB online application

Awamu ya kwanza Majina ya Wanafunzia walipata mikopo na ruzuku yenye jumla ya wanafunzi 135,240

by Mr Uhakika
October 24, 2025
0

426.5 BILIONI ZATOLEWA KWA WANAFUNZI 135,240 Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) leo Ijumaa, Oktoba 24,2025 imetoa awamu ya kwanza ya upangaji mikopo na...

Maombi ya mkopo HESLB OLAMS – Online Loan Application 2025/26 – HESLB online application

Orodha ya Majina Ya Waliopata Mkopo HESLB Batch 1, 2 & 3 – Pakua PDF 2025/26

by Mr Uhakika
October 15, 2025
0

Unatafuta majina ya waliopata mkopo wa HESLB kwa mwaka wa 2025/26? Usihangaike tena! Tumekusanya orodha kamili itakayopatikana kwa urahisi na awamu katika fomati ya PDF. Usipoteze muda kutafuta...

Maombi ya mkopo HESLB OLAMS – Online Loan Application 2025/26 – HESLB online application

HESLB Majina ya Waliopata Mkopo 2025 – Mikopo ya Wanafunzi wa Stashahada kwa Wanufaika

by Mr Uhakika
October 14, 2025
0

Katika mwaka wa 2025, wanafunzi wengi wa stashahada wamepata mkopo kutoka katika shirika la elimu ya juu nchini. Huu ni wakati wa furaha na matumaini kwa wanufaika hawa,...

Maombi ya mkopo HESLB OLAMS – Online Loan Application 2025/26 – HESLB online application

Jinsi Ya kurekebisha Makosa ya kuomba mkopo HESLB

by Mr Uhakika
June 23, 2025
0

Makosa ya kujaza au kuomba mkopo HESLB (Higher Education Students' Loans Board) ni kawaida kutokea na wanafunzi wengi hukumbana nayo. Hapa chini ni mwongozo wa jinsi ya kurekebisha...

Load More
Next Post
IFM

IFM online application; Jinsi ya kufanya maombi ya chuo cha IFM 2025/2026

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

No Result
View All Result
  • Home
  • MICHEZO
    • Mikeka ya leo
  • AJIRA KAZI
  • NYIMBO MPYA YA
  • ELIMU
    • JKT selection
    • Form One Selections
    • form five selections
    • NECTA Form Six Results
    • NECTA Standard Seven Results

© 2025 Uhakika News