Bodi ya Ligi Kuu nchini Misri imempiga adhabu mshambuliaji wa klabu ya Pyramids FC Fiston Mayele ya kutocheza mechi moja na kulipa faini ya Paundi elfu tano za Misri.
Mchezaji huyo wa Kimataifa wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo alioneshwa kadi yake ya tatu ya njano msimu huu wakati Pyramids FC ilipochapwa 4-2 na National Bank siku ya Ijumaa Mei 9, 2025 katika Ligi Kuu Misri.
Mshambulizi huyo anatarajiwa kuukosa mchezo ujao dhidi ya Zamalek Mei 13, 2025.
Comments