➡️Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo wa Tanzania , Profesa Palamagamba Kabudi anatarajiwa kukutana na viongozi wa Simba Sports Club na Young Africans kuzungumzia sakata la uamuzi wa Simba kugomea mechi ya watani wa jadi iliyokuwa ifanyike Machi 8, 2025 kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam.
➡️Wengine ambao wanatarajiwa kushiriki kikao hicho kilichopangwa kufanyika Machi 27 mwaka huu ni viongozi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) pamoja na viongozi kutoka bodi ya Ligi Kuu ya Tanzania (TPBL).
➡️Timu ya Simba Sports Club iligomea mchezo huo kwa madai ya ukiukwaji wa Kanuni namba 17(45) ya Kanuni za Ligi Kuu Tanzania Bara, ambayo inaruhusu timu ngeni kufanya mazoezi kwenye uwanja wa mechi angalau mara moja kabla ya siku ya mechi.
Comments